Wednesday, 2 November 2016

Ratiba ya michezo ya UEFA leo Jumatano November 2

Baada ya kushuhudia Man City akimnyoosha Barcelona hapo jana katika uwanja wake wa nyumbani, tuna nafasi nyingine tena ya kukiangalia atakachokifanya Bayer Leverkusen nyumbani kwa Tottenham Hotspurs. Ni baada ya mchezo uliopita baina ya timu hizo kumalizika kwa sare ya bila kufungana.
Na huo ni mmoja tu kati ya michezo 8 ambayo inatarajiwa kupigwa usiku wa leo katika viwanja tofauti tofauti ili kukamilisha idadi ya michezo 4 katika kila timu kwa hatui hii ya makundi ya Ligi ya mabingwa barani humo.
Na ratiba ya michezo hiyo ipo kama ifuatavyo.
Group E
  1. Monaco vs CSKA Moscow
  2. Tottenham Hotspurs vs Bayer Leverkusen
Group F
  1. Borussia Dortmund vs Sporting CP
  2. Legia Warszawa vs Real Madrid
Group G
  1. FC Koebenhavn vs Leicester City
  2. FC Porto vs Club Brugge
Group H
  1. Juventus vs Lyon
  2. Sevilla vs Dinamo Zagreb
Michezo yote hiyo itachezwa mishale ya saa 4:45 Usiku.

This Is The Newest Post


EmoticonEmoticon