Wednesday, 2 November 2016

Ratiba ya michezo ya UEFA leo Jumatano November 2

Baada ya kushuhudia Man City akimnyoosha Barcelona hapo jana katika uwanja wake wa nyumbani, tuna nafasi nyingine tena ya kukiangalia atakachokifanya Bayer Leverkusen nyumbani kwa Tottenham Hotspurs. Ni baada ya mchezo uliopita baina ya timu hizo kumalizika kwa sare ya bila kufungana.
Na huo ni mmoja tu kati ya michezo 8 ambayo inatarajiwa kupigwa usiku wa leo katika viwanja tofauti tofauti ili kukamilisha idadi ya michezo 4 katika kila timu kwa hatui hii ya makundi ya Ligi ya mabingwa barani humo.
Na ratiba ya michezo hiyo ipo kama ifuatavyo.
Group E
  1. Monaco vs CSKA Moscow
  2. Tottenham Hotspurs vs Bayer Leverkusen
Group F
  1. Borussia Dortmund vs Sporting CP
  2. Legia Warszawa vs Real Madrid
Group G
  1. FC Koebenhavn vs Leicester City
  2. FC Porto vs Club Brugge
Group H
  1. Juventus vs Lyon
  2. Sevilla vs Dinamo Zagreb
Michezo yote hiyo itachezwa mishale ya saa 4:45 Usiku.

Madini mapya yagunduliwa Mererani, Tanzania

Madini mapya yamegunduliwa nchini Tanzania, katika eneo lenye madini ya kipekee la Manyara, na kupewa jina Merelaniite.

Jina hilo limetokana na eneo ambalo madini hayo yalipatikana, Merelani (Mererani) katika milima ya Lelatema katika wilaya ya Simanjiro katika eneo la Manyara.
Eneo hilo linafahamika sana kwa madini ya Tanzanite.
Madini hayo yaligunduliwa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Kiteknolojia cha Michigan cha Marekani, makavazi ya historia asilia ya London, chuo kikuu cha Di Firenze cha Italia na makavazi ya historia asilia ya Smithsonian ya Washington.
Wataalamu sita waliofanya uchunguzi, kwenye makala iliyochapishwa kwenye jarida la Minerals (Madini) wanasema madini hayo yana vipande vinavyofanana na sharubu vya rangi ya kijivu vya urefu wa milimita moja hivi, ingawa kuna baadhi vyenye urefu wa hadi mililita 12.
Kipenyo cha vipande hivyo ni mikrometa kadha.
Madini hayo yanakaribiana na madini ya zoisite (aina ya tanzanite), prehnite, stilbite, chabazite, tremolite, diopside, quartz, calcite, graphite, alabandite na wurtzite.
"Madini haya mapya yametambuliwa na taasisi inayoyapa majina madini, IMA CNMNC (2016-042), na kupewa jina linalotokana na eneo yalipogunduliwa kwa heshima ya wachimba migodi wa eneo hilo wa zamani, wanaoishi na wanaofanya kazi," makala ya wataalamu hayo inasema.
"Wilaya ya Merelani imekuwa maarufu tangu mwishoni mwa miaka ya 1960 kutokana na aina ya madini ya thamani ya rangi ya samawati kwa jina zoisite yafahamikayo kama tanzanite, lakini ni eneo muhimu sana kwa wanaotafuta madini ya kipekee na ni eneo la kusisimua sana kutafuta madini mapya," John Jaszczak, mwanafizikia katika Chuo Kikuu cha Kiteknolojia cha Michigan, na aliyeongoza katika kuandika makala kuhusu ugunduzi wa madini hayo anasema.
Madini hayo yalitambuliwa mara ya kwanza mwaka 2012 na Simon Harrison na Michael Wise, bila wataalamu hao kuyafahamu vyema, pale walipogundua vitu vilivyoonekana kama nyaya ndogo zilizokuwa zimedunga na kuingia ndani ya vipande vya madini ya chabazite.
Baadaye uchunguzi zaidi ulifanywa na ikagunduliwa kwamba yalikuwa madini tofauti.
Mshirikishe mwenzako Unavyoweza kumshirikisha mwenzako.

Huyu Ndio Mwanamuziki wa Bongo Flava Mwenye Mafanikio Makubwa zaidi Kuliko Wanamuziki Wote Tanzania

Anaitwa AMBWENE YESSAYA AKA AY ni mmoja wa wasanii ambaye ana mafanikio makubwa sana kimuziki kuliko msanii yeyote yule hapa nchini Tanzania,vile vile yeye ndiye msanii wa kwanza Tanzania kuipeperusha bendera ya Tanzania katika anga za kimataifa mpaka ulaya.Historia yake ya muziki ilianzia miaka 1998

-Pesa yake ya kwanza kurekodi ngoma studio alipewa na mama yake Tshs 20000/=
-Ni mkulima (ana mashamba ya mpunga zaidi ya heka 100 huko ifakara Morogoro
-Ni mjasiriamali mwenye biashara nyingi ikiwemo duka la nguo
-Ni mmiliki wa vipindi vya TV vya MKASI na NGAZI KWA NGAZI vinavyorushwa EAST AFRICA TV

-Anamiliki kampuni ya UNITY ENTERTAINMENT inayojihusisha na uwakala wa kazi za sanaa,matangazo na kuunganisha wasanii,pia kuleta wasanii wa nje.

Mbeya Waibwaga Yanga Sokoine 2-1, Vurugu Zatawala

MBEYA City Council FC imeutumia vizuri Uwanja wa nyumbani, Sokoine mjini Mbeya baada ya kuwafunga mabingwa watetezi, Yanga mabao 2-1.

Ushindi huo wa kwaza kwa Mbeya dhidi ya Yanga tangu wapande Ligi Kuu, unaifanya MCC ifikishe pointi 19 baada ya kucheza mechi 14, wakati Yanga inabaki na pointi zake 27 za mechi 13.

Mbeya City waliuanza vizuri mchezo na kufanikiwa kumaliza kipindi cha kwanza wanaongoza kwa mabao 2-1.

Beki wa kushoto wa MCC, Hassan Mwasapili aliifungia timu yake bao la kwanza dakika ya sita baada ya kumtungua vizuri kipa wa Yanga, Deo Munishi ‘Dida’ kwa shuti la mbali la mpira wa adhabu.

Nahodha Kenny Ally akaifungia Mbeya City bao la pili dakika ya 36 kwa shuti la mbali pia baada ya kuanzishiwa mpira wa adhabu na beki wa kulia Haruna Shamte, aliyechezewa rafu na beki wa Yanga, Hassan Kessy.

Bao hilo lilizua utata baada ya wachezaji wa Yanga kumfuata refa Rajab Mrope wa Ruvuma kulikubali, kulikataa baada ya kuzongwa na wachezaji na Yanga na kulikubali tena baada ya majadiliano na wasaidizi wake.

Lakini kilichoonekana ni wachezaji wa Yanga walikuwa wamezubaa hawakujipanga na Shamte akatumia mwanya huo kumuanzishia mfungaji haraka, ambaye aliunganishia shuti nyavuni.

Wachezaji wa Mbeya City wakamvamia refa huyo na wakati huo huo mashabiki wao waliingia uwanjani na wengine walikuwa wakirusha chupa za maji kutoka jukwaani, hadi amani ikachafuka uwanjani.

Wakati huo huo refa huyo alikuwa akizongwa na wachezaji wa Mbeya City na ghafla akageuka na kulibariki hilo, hivyo mchezo kuendelea.

Mshambuliaji Mzimbabwe, Donald Ngoma akaifungia Yanga bao la kwanza dakika ya 45 baada ya kuwatoka mabeki wa Mbeya City na kumtungua kipa Mmalawi Owen Chaima.

Kipindi cha pili, kocha Mholanzi wa Yanga, Hans van der Pluijm alianza kumpumzisha kiungo wa ulinzi, Mbuyu Twite na kumuingiza Mzimbabwe, Thabani Kamusoko kabla ya baadaye kumtoa winga Deus Kaseke na kumuingiza Geoffrey Mwashiuya.

Katika kipindi hicho cha pili, Kocha Mmalawi wa Mbeya City alionekana kubadilisha mbinu na kuamua kucheza mchezo wa kujihami kuulinda ushindi wao, hivyo kuwapa kazi Yanga ya kuupasua ukuta wao.

Kinara wa mabao wa Yanga, Amissi Joselyn Tambwe hakuwa katika siku nzuri leo baada ya kukosa bao wazi dakika ya 64 akiunganishia nje kwa kichwa krosi ya Ngoma.

Mbeya City waliendelea kucheza kwa kujihami hukui wakipeleka mashambulizi ya kushitukiza langoni mwa Yanga hadi kipyenga cha mwisho.

Wachezaji wa Yanga wakamvaa tena refa wakidai amemaliza mchezo kabla ya muda, hivyo kusababisha atolewe uwanjani kwa msaada wa Jeshi la Polisi.

Kikosi cha Mbeya City kilikuwa; Owen Chaima, Haruna Shamte, Hassan Mwasapili, Sankhani Mkandawile, Rajab Zahir, Tumba Lui, Raphael Daud, Kenny Ally, Ditram Nchimbi, Hamedy Murutabose/Omary Ramadhani dk18 na Joseph Mahundi/Issa Nelson dk90+.

Yanga; Deo Munishi ‘Dida’, Hassan Kessy, Mwinyi Haji Mngwali, Andrew Vincent, Vincent Bossou, Mbuyu Twite/Thabani Kamusoko dk46, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Amissi Tambwe/Obrey Chirwa dk68, Donald Ngoma na Deus Kaseke/Geoffrey Mwashiuya dk51

Simba Kasi Zaidi Kuuelekea Ubingwa, Stand United Yafa 1-0 Kambarage

SIMBA SC wameendelea kulifukuzia kwa kasi taji la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya timu ngumu msimu huu, Stand United ya Shinyanga.

Ushindi huo, unaifanya Simba SC ifikishe pointi 35 baada ya kucheza mechi 13, wakati Stand inabaki na pointi zake 22 za mechi 14.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na marefa, Shomary Lawi wa Kigoma aliyesaidiwa na Mirambo Tshikungu na Robert Ruhemeja, Simba walipata bao lao mapema kipindi cha kwanza.

Bao hilo lilifungwa na winga machachari wa Wekundu hao wa Msimbazi, Shizza Ramadhani Kichuya kwa penalti dakika ya 33 baada ya mshambuliaji Mrundi, Laudit Mavugo kuangushwa na beki Adeyum Ahmed kwenye boksi.

Baaada ya bao hilo, timu hizo ziliendelea kushambuliana kwa zamu, lakini ni Simba SC waliokuwa waking’ara uwanjani.

Mapema dakika ya nane, Kichuya aliunganishia nje kwa kichwa krosi ya beki Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ kabla ya Nahodha wa Stand United, Jacob Massawe kupiga juu kufuatia krosi ya Frank Hamisi.

Kipindi cha pili, mchezo uliendelea kuwa wa mashambulizi ya pande zote mbili, lakini Simba inayofundishwa na Mcameroon, Joseph Marius Omog ilifanikiwa kuulinda ushindi wake.

Na Simba SC ilikaribia kupata bao la pili dakika ya 65 kama si kiungo Mohamed ‘Mo’ Ibrahim kupiga juu ya lango kufuatia pasi nzuri ya Kichuya.

Kikosi cha Stand United kilikuwa; Frank Muwonge, Aaron Lulambo, Adeyum Ahmed, Erick Mlilo, Ibrahim Job, Pastory Athanas, Kelvin Kongwe, Jacob Massawe, Suleiman Kassim ‘Selembe’, Frank Hamisi na Amri Kiemba.

Simba SC; Vincent Angban, Janvier  Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Method Mwanjali, Juuko   Murshid, Jonas Mkude, Shizza Kichuya/Jamal Mnyate dk75, Muzamil Yassin, Laudit  Mavugo/Ibrahim Hajib dk87, Mohammed ‘Mo’ Ibrahim na Mwinyi Kazimoto/Mussa Ndusha dk79.

Nchi 5 nje ya Afrika zenye vijana wengi ambao hawasomi na hawana kazi


Ni orodha kutoka mtandao wa OECD Data uliozitaja nchi tano duniani zenye idadi kubwa ya watu ambao hawasomi, hawana mafunzo ya aina yoyote na hawana kazi.
Data za watu hao zinaonyesha vijana wenye umri wa miaka 20 mpaka 24 ndio wamekuwa wengi zaidi kwenye idadi hiyo, hii ni ripoti ambayo utafiti wake umefanyika mpaka 

 Nchi ya kwanza inayoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ni Italia, namba mbili ni Uturuki, ya tatu ni Ugiriki ikifuatiwa na Hispania kisha Mexico kama inavyoonekana kwenye hii orodha hapa chini.





Monday, 31 October 2016

TOP 10: Wachezaji wanaolipwa mshahara mkubwa duniani, Afrika ni mmoja tu

Staa wa kimataifa wa Wales anayeichezea klabu ya Real Madrid ya Hispania Gareth Bale ameingia katika TOP 3 ya wachezaji wa soka wanaolipwa pesa ndefu zaidi duniani ambapo ameingia katika list hiyo kutokana na mkataba wake mpya na Real Madrid.



Gareth Bale
Kwa sasa Bale atakuwa akilipwa pound 346,000 kwa wiki ambazo ni zaidi ya Tsh milioni 900 ambapo katika kipindi cha miaka sita Bale atakuwa kaingiza jumla ya pound milioni 108.


Yaya Toure
Bale sasa anakuwa katika TOP 3 hiyo wakati kwa wachezaji wa Afrika, kiungo wa Man City na raia wa Ivory Coast Yaya Toure yupo nafasi ya 10 katika list ya wachezaji wanaolipwa mshahara mkubwa duniani licha ya kuwa yupo katika wakati mgumu wa kujua hatma yake chini ya Guardiola.